Psalms 35:1-8

Kuomba Msaada: Kuokolewa Kutokana Na Maadui

Zaburi ya Daudi.

1 aEe Bwana, pingana na wale wanaopingana nami,
upigane na hao wanaopigana nami.
2 bChukua ngao na kigao.
Inuka unisaidie.
3Inua mkuki wako na fumo
Fumo ni sawa na sagai, maana yake ni mkuki mfupi.
lako
dhidi ya hao wanaonifuatia.
Iambie nafsi yangu,
“Mimi ni wokovu wako.”

4 dWafedheheshwe na waaibishwe
wale wanaotafuta uhai wangu.
Wanaofanya shauri kuniangamiza
warudishwe nyuma kwa hofu.
5 eWawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,
malaika wa Bwana akiwafukuza.
6Njia yao na iwe giza na ya utelezi,
malaika wa Bwana akiwafuatilia.
7 fKwa vile walinifichia wavu wao bila sababu,
na bila sababu wamenichimbia shimo,
8 gmaafa na yawapate ghafula:
wavu walionifichia na uwatege wenyewe,
na waanguke katika shimo hilo,
kwa maangamizo yao.
Copyright information for SwhNEN